Saturday, April 4, 2015

KENDRICK LAMAR ATHIBITISHA UHUSIANO WAKE NA MPENZI WAKE WA ZAMANI AMBAYE ALIKUWA



Kendrick Lamar athibitisha uhusiano wake Na mpenzi wake wa zamani ambaye alikuwa aki toka naye kimapenzi tangu walipokuwa high school lakini hivi sasa inasemekana wanampango wa kuoana rasmi.

Kendrick Lamar's  ambaye hivi sasa album yake ya To Pimp a Butterfly  inaendelea kusumbua kwenye   Billboard chati  200 kwa zaidi ya wiki ya pili sasa , lakini rapper huyo kutoka mjini Compton mapema jana alizungumzia kuhusiana na uhusiano wake na mkewe mtaarajiwa Whitney Alford  kwamba si habari  mbaya mahusiano yao yakiwekwa bayana nafikiri ni habari njema  katika maisha yangu . Kendrick Lamar‘s alijikuta amezama kwenye penzi la mtoto Whitney Alford msichana ambaye walisoma wote enzi hizo tangu wakiwa high school.
Kendrick amethibitisha hayo alipokuwa akihojiwa na kituo cha radio kwenye kipindi cha breakfast  club jana asubuhi jijini New York , mtangazaji wa kipindi hicho alimuuliza swali Kendrick lamar jee  ni kweli kuna uhusiano wowote uliopo kati yake yeye na Whitney Alford akajibu ni kweli sio siri tena nafikiri unafahamu hilo, Kendrick lamar akamaliza kwa kusema “I'm loyal to the soil” Na hatimaye siku ya mwisho tunataka watu wafahamu kwamba kumbe tunaishi na watu wenye malengo haijalishi ni mwanaume au ni mwanamke jamii yote inayokuzunguka inapaswa kufahamu hilo.

Lakini ikumbukwe kuwa Kendrick amewahi kuhojiwa mwezi January na mmoja wanao host kipindi cha Billboard na kuulizwa swali kuhusu Whitney Alford je ni mpenzi wake au raha? kwa bahati mbaya au nzuri alikataa kata kata alisema ni rafiki yangu  wakike hakuna kingine zaidi ya hicho.  Naweza sema ni rafiki yangu tulifahamiana tukiwa wote shuleni kwa namna nyingine naweza kumuita ni zaidi ya rafiki.


Jina lake halisi anaitwa Kendrick Lamar Duckworth alizaliwa tarehe 17 mwezi june mwaka 1987 anafahamika kama   Kendrick Lamar, ni msanii wa miondoko ya HipHop akitokea mjini Compton, jijini California. Mwaka 2004, Lamar alisaini mkataba na kuwa chini ya label ya   Top Dawg Entertainment (TDE).  Baadaye tena Lamar alisaini mkataba na studio mbili tofauti hii ilikuwa mwaka   2012, pale ambapo aliingia rasmi kwenye studio za Aftermath na Interscope Records.  
Ukiachana na kazi yake ya mziki, Lamar  amewahi kuwa  mwanachama wa kundi la Black Hippy na baadaye kundi hilo kuitwa Super Group  kipindi hicho akiwa baado mdogo kundi hilo lilifahamika sana na kujipatia umaarufu kote duniani.
kwa maelezo yake anasema Super Group  ni kundi ambalo lina wasanii wa hiphop wanaotokea  kwenye ukanda wa Magharibi Na Kusini Mwa Los Angeles wasanii wote walikuwa chini ya label ya  Top Dawg Entertainment {TDE} hakuwa pekee yake bali alikuwa na wasanii wenzake kama vile  Schoolboy Q, Jay Rock, na  Ab-Soul.


Umaarufu wake na kazi zake  ndiyo zilizomfanya akutane na wasanii wakongwe wa Hip Hop kutoka nchini marekani na hatimaye aliweza kufanya nao kazi mbali mbali  miongoni wa wasanii hao ni  Dr. Dre, The Game, Eminem, Drake, Young Jeezy, Talib Kweli, Busta Rhymes, E-40, Warren G, na  Lil Wayne ndipo alipoanza kuona soko la muziki  wa Hip Hop jinsi lilivyo na unatakiwa kufanya nini ili uweze kuyafikia malengo yako.

kingine kipya fahamu ya kwamba album iliyomtoa Lamar's kwenye mziki ni ile ya , Good Kid, M.A.A.D City, aliyoiachia rasmi  October mwaka 2012 na kusambazwa duniani kote. Album hiyo ilikuwa na zile nyimbo kali ambazo zilipata nafasi ya kuingia kwenye orodha ya Top 40 hits miongoni mwa nyimbo hizo ni  "Swimming Pools (Drank)", "Bitch, Don't Kill My Vibe", na ile ya  "Poetic Justice".  Baada ya kuachia album hiyo ilipewa shavu na kushika nafasi ya pili kwenye US Billboard 200 chart na baadaye iliweza kuthibitishwa na hatimaye kuwa  miongoni mwa album ambazo zimeingia kwenye orodha ya Platinum kwa mjibu wa (RIAA).

Album yake ya kwanza kutoka ilikuwa ni Youngest Head Nigga In Charge mwaka 2003, ikifuatiwa na C4 mwaka 2009, ikaja Overly Dedicated mwaka 2010, Section mwaka 2011 lakini zilizo hit na kutikisa vituo vya luninga na vituo vya radio ni ile ya Good Kid M.A.A.D City ya mwaka 2012 na hii mpya ya To Pimp A Butterfly aliyoitoa mapema mwezi march mwaka huu wa 2015.

Mapema mwaka  2013 kituo kikubwa na maarufu cha luninga  cha MTV Base kilimtunuku Kendrick Lamar kuwa msanii chipukisi namba moja kwenye mziki wa hip hop na   kwenye tuzo za MTV orodha ya awali inadhihirisha Lamar amepokea jumla ya tuzo saba  za Grammy  katika kinyang’anyiro hicho akiwa kama  Best New Artist, Album of the Year na  Best Rap Song hiyo ilikuwa mwaka 2014. Na mwaka 2015 aliweza kushinda tuzo 2 ambazo ni  A Best Rap Performance na  Best Rap Song for his single.

No comments:

Post a Comment