Ijumaa ya leo ni siku ya kumkumbuka aliyewahi kuwa
muasisi wa taifa ya afrika ya kusini ambaye kwa sasa ni hayati wengi tuna
mfahamu kwa jina la madiba lakini jina lake halisi ni Nelson Rolihlahla Mandela alizaliwa July 18, 1918 Mvezo, jimbo la Cape
town na kufariki
December 5 mwaka 2013 akiwa na umri wa
miaka 95 huko nchini afrika ya kusini, Johannesburg.
Atakumbukwa kwa
mema aliyowafanyia wananchi wa afrika ya kusini na duniani kote kwa kutetea
haki za kibinadamu , ubaguzi wa rangi ambao kwa kiasi kikubwa lilikuwa ni janga
kubwa mno kwenye taifa hilo.

Alishika wadhifa
wa kuwa rais wa kwanza nchini Afrika ya Kusini mwaka 1994 mpaka 1999 ni mwanasiasa,
mwanamapinduzi, mwanafasafa, lakini pia amewahi kuwa mtendaji mkuu wa kwanza wa
afrika ya kusini na alichaguliwa kuwa Rais kwa uchaguzi sahihi tena wa
kidemokrasia na hakuna aliyepinga kuhusu hilo.
Serikali yake
ilijikita zaidi kwenye masuala ya kutokomeza umasikini, ubaguzi wa rangi, mambo
ya urasimu. Hivi hapa ni baadhi ya Vyama vya siasa ambavyo amewahi kuvitumikia
enzi za uhai wake chama cha siasa cha taifa la Afrika ya Kusini na ujamaa wa
kidemokrasia alikitumikia akiwa kama Rais wa chama cha (ANC) yaani African
National Congress kuanzia mwaka 1991 hadi 1997 Nelson Mandela ambaye maisha
yake alijitoa muhanga kwa kila jambo pale ambapo aliamua kupigania huru wa nchi
yake huku akiwa na nia njema tuu lakini pia
sheria, misingi ya utu wa
kibinadamu ifuatwe. Lakini pia aliwahi kushika wadhifa wa kuwa katibu mkuu wa
(NAM) yaani Non-Aligned Movement kuanzia mwaka 1998 hadi 1999.
Siku hii ya leo ni nafasi pekee ya kuchukua atua kwa
vitendo kwa kufanya uombolezaji kutokana na jitahada zake alizozifanya enzi za
uhai wake ikiwa pamoja na kukubari mabadiliko aliyoyafanya na wengi kuvutiwa
karibu kila pembe ya dunia,tumia angalau dakika kadhaa kuhamasisha ulimwengu na
kuwaombea/kuwasihi wengine .
Alikulia kwenye kijiji cha Xhosa na alipata bahati ya kuzaliwa katika familia
bora ambayo waliita kwa jina la Thembu, Mandela alipata fursa ya kusoma chuo kikuu
cha Fort Hare na
baadaye alijiunga na chuo kikuu cha Witwatersrand, wakati huo alikuwa anasomea sheria
.Aliishi Johannesburg, alianza kujishugurisha na siasa za kikoloni
, na ndipo alipopata fursa ya kujiunga na chama cha ANC na kuwa ni miongoni mwa
mwanachama ambaye aliweza kuwa muasisi wa kundi la Youth League . Baada ya
chama cha ASANP kushika madaraka mwaka
1948 kilikuwa na nguvu mno , mzee Nelson Mandela alianza kupoteza matumaini
akidhani ya kwamba hapo baadaye chama chake cha ANC kamwe hakitoweza kuja
kushika wadhifa wowote ule nchini humo lakini hakukata tamaa mwanzoni mwa mwaka
1952 alianzisha kampeni zake baadaye
aliteuliwa na wanachama wake kugombea baadhi ya nyadhifa kupitia moja la shirika lisilo la kiserikali
la Transvaal na alitumikia mpaka mwaka 1955. Alifanya kazi akiwa kama mwanasheria, alianza
kuzipitia upya baadhi ya shughuri ambazo zilikuwa zikifanywa na ANC.
Mandela alitumikia kifungo cha jela kwa mda wa miaka 27
miongoni mwa magereza ambayo amewahi kuyatumikia ni Robben Island, baadaye huko Pollsmoor
na Victor Verster . Alitoka jela mwaka 1990 wakati ule ambao nchi
ya afrika ya kusini ilikuwa katika mgogoro mkubwa sana .
Mandela baada ya kutoka jela aliungana na mtu wake wa
karibu ambaye alikuwa ni Rais pia ndugu F.
W. de Klerk ili
kukomesha vitendo vilivyokuwa vinaenda kinyume na vile anavyoishi
binadamu,kuimarisha hali ya usalama wa taifa lao na hatimaye kuitisha uchaguzi
mwaka 1994.
Nafasi iliyomfanya asimame kidedea kuwania urais na
hatimaye kushinda kwa kishindo kuwa Rais wa kwanza mweusi nchini Afrika ya
Kusini na hakuna aliyeamini mpaka pale walipochapisha kwenye baadhi ya
magazeti,vituo vya redio kutangaza na vituo vya luninga kurusha moja kwa moja kilichokuwa
kinaendelea kwenye uchaguzi huo.
Alioa mitara waswahili wanasema hivyo, lakini wenzetu wazungu
wanaita “monogamy” Mke wake wa kwanza anaitwa Evelyn
Ntoko Mase (ambaye
waliishi naye kuanzia mwaka 1944 na walitarakiana mwaka 1957) wapili ni Winnie Madikizela (ambaye waliishi naye kuanzia mwaka 1958 na walitarakiana mwaka 1996) watatu na wa mwisho alikuwa ni Graça
Machel (ambaye
waliishi naye kuanzia mwaka 1998–2013 mpaka umauti unamkuta)
Nelson
Mandela mpaka anafariki ameacha watoto sita tuu ambao ni :
Thembekile
Mandela,Makaziwe Mandela,Makgatho Mandela,Makaziwe Mandela, Zenani
Mandela na Zindziswa Mandela
Akiendelea na majukumu yake ya kila siku
kama rais muasisi wa taifa hilo aliweza tena kuanzisha baraza la kutetea
ukombozi wa sera ya uchumi , utawala wake/uongozi wake uliwenza kutanguliza upya na uanzishwaji wa sheria ya
aridhi ambapo kila mwananchi alipata nafasi ya kumilikishwa aridhi kupitia
sheria hiyo, si hivyo tuu walianzisha tena sheria ya kuzuia na kumbambana na rushwa, sheria ya
kuhakikisha kila mwananchi anapata elimu bora kujengwaa kwa kasi vyuo
vikuu,shule za sekondari,vyuo vya ufundi na shule za awali, huduma bora za afya
kama vile upatikanaji wa hospitali,vituo vya zahanati na kadhalika,upatikanaji
wa lishe bora,ujenzi wa miundo mbinu ya barabara,reli,anga na majini. Ujenzi wa
viwanda vikubwa uwekezaji wenye manufaa kwa taifa husika.
No comments:
Post a Comment